Mwongozo Alioutoa Mtume ﷺ kwa Sufyan ibn Abdillah Ath-Thaqafi
Sufyan ibn Abdillah Ath-Thaqafi (Mwenyezi Mungu awe radhi naye) alisema: Niliuliza, "Ya Rasuliullah! Niambie jambo ambalo nitalishikilia kwa nguvu." Mtume ﷺ akajibu, "Sema, 'Mola wangu ni Allah,' kisha uwe imara." Nikasema tena, "Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu! Unaniogopea nini zaidi?" Mtume ﷺ akashika ulimi wake mwenyewe na kusema, "Huu." [Hadith imesimuliwa na Tirmidhi, naye akaisifu kuwa ni Hasan Sahih]